Kiswahili 35. “Divai Safi na Takatifu” -au- “Mvinyo wa Babeli”

BISMILA-HIR RAHMA-NIR RAHIM

Asalamu Aleikum!

 

Siku hizi watu wengi wamechanganyikiwa…wamechanganyikiwa kwa kunywa sana vileo ambavyo havikukusudiwa kunywewa na wanadamu. Kwa sababu Ibilisi anazidanganya akili na mioyo ya watu, kwa kileo kilichochachuka, wengi hufanya maamuzi ambayo wasingefanya kama wangekuwa na akili safi. Maelfu huingia katika maangamizi wanapoyatupilia mbali mauidha ya Mwenyezi Mungu. Hakuna ajabu yo yote, mafundisho hayo yanayoeleweka wazi yametolewa katika Kurani Tukufu na katika Vitabu Vitakatifu vya Taurati na Injili ya kuwa divai iliyochachuka au kileo hakipaswi kunywewa kama kinywaji cha mwanadamu. Kwa rehema Mwenyezi Mungu anajaribu kutuonya juu ya hatari hiyo.
“…Wanakuuliza juu ya ulevi na kamari … katika hivyo mna madhara makuu…” Sura 2:219 Al Baqarah

“…Kunywa mvinyo hakuwafai wafalme; wala haifai wakuu waseme, Ki wapi kileo?” Mithali 31:4 Taurati

“…Mola wao atawanywesha kinywaji safi kabisa.” Sura 76:21 Ad-Dahr

Iko divai iliyo safi na takatifu, ni juisi safi ya mizabibu au tunda jinginelo lote. Ni juisi isiyochachuka ya matunda iliyokusudiwa kuwa baraka kwa wanadamu.
“BWANA asema hivi, kama vile divai mpya ipatikanavyo katika kichala, na mtu mmoja husema, usikiharibu kwa maana mna baraka ndani yake…” Taurati Isaya 65:8

Ibilisi amemdanganya mwanadamu kutengeneza kileo ambacho kinafanya akili na mioyo ya watu wengi kuchanganyikiwa na kuharibika. Tungekuwa na busara kwa kuyazingatia mauidha yatokayo katika Vitabu Vitakatifu. Masihi Isa alipopewa siki akiwa anapata maumivu makali sana juu ya chombo kile cha kikatili cha kunyongea watu, alipewa siki, lakini alipoionja na kujua ni siki alikataa kuinywa hata katika hali yake ile ya kuteseka.
“Wakampa kunywa divai iliyochanganyika na nyongo; lakini yeye alipoionja hakutaka kunywa.” Injili Mathayo 27:34
Ni kielelezo bora kilichoje hicho ambacho tunacho kutoka kwa Masihi Isa kitufanyacho tukatae cho chote kilichochafuliwa.

Kikombe Hadaa cha Mashetani

Walakini uko mvinyo mwingine, ambao una madhara makubwa zaidi, unafisha, na kuhadaa kuliko mvinyo wenye kileo. Mvinyo huo unaongelewa juu yake katika Vitabu Vitakatirfu vya Biblia, Taurati na Injili. Hakika mvinyo huo umetengenezwa kutoka katika mashamba ya mizabibu ya Shetani mwenyewe, unaitwa “Kikombe cha Mashetani”.
“Hamwezi kunywea kikombe cha Bwana na kikombe cha mashetani.” 1 Wakorintho 10:20,21

Mvinyo huu ni mchanganyiko wa mafundisho ya kweli na ya uongo au mafundisho potofu ambayo yanafanywa yaonekane kuwa ya kweli . Gilasi nyingi za mvinyo huonekana kuwa safi, mpaka hapo unapouonja. Na, halafu, ukiisha uonja mara nyingi huwa mchungu na mtamu kwa namna inayohatariisha na wapaswa kukataliwa. Mvinyo huo huja ukiwa na ladha inayotia uchungu na kuuma, maana rangi yenyewe tu haiwezi kuudhihirisha mvinyo huo kama ni safi au umechafuliwa. Hivyo ndivyo ilivyo kuhusu mafundisho ya dini. Ni lazima yachunguzwe ili kuona kama mafundisho hayo ni matakatifu au yamechafuliwa. Kwa kila kweli moja ya Mwenyezi Mungu, Ibilisi au Shetani ameweka fundisho lake la uongo na linaonekana kana kwamba ni la kweli , lakini ladha yake ni ya ufisadi na kama mvinyo huo ukinywewa mara nyingi matokeo ni maangamizi.

Twahitaji kuwa na hekima ya kukataa ule uliochafuliwa na kupokea ule ulio safi na mtakatifu. Hivyo ndivyo yalivyo na mafundisho au mafundisho ya dini. Kuna yale yaliyo safi na matakatifu ambayo yanaelekeza kwenye uzima wa milele, kisha yapo yale yaliyochafuliwa na yasiyo safi ambayo huelekeza kwenye maangamizi na kifo.
Ibilisi hunyosha mkono wake ulioshika kikombe cha mashetani kwa kila mmoja wetu kwa njia mbalimbali akijaribu kutushawishi tunywe. Tuna haja ya kuonywa juu ya hila zake. Hili ndilo kusudi la kipeperushi hiki kidogo unachokishika mkononi mwako. Mwenyezi Mungu kwa rehema anamjulisha mtu anayetega sikio lake kusikiliza juu ya utendaji kazi wa siri wa Ibilisi. Upendo wa Mwenyezi Mungu kwa watu ni wa namna ile anayotaka wote wawe macho na kuchukua hadhari dhidi ya hila zake Shetani.

Mvinyo wa Babeli

Mpaka hapa tunataka kuangalia yaliyo ya kweli na yale ya uongo. Taurati na Injili ina mengi ya kusema juu ya mafundisho ya uongo ambayo kwayo Ibilisi amekuwa akiwaongoza mamilioni ya watu. Leo tunataka kuyaweka peupe mafundisho hayo mengi ya uongo na kuyaelezea yale ya kweli kutoka katika Kitabu. Unabii wa kale wa Injili unasema juu ya wakati fulani katika siku hizi za mwisho yatakapopokewa yale ya uongo badala ya yale yaliyo safi.… “Maana utakuja wakati watakapoyakataa mafundisho yenye uzima; na kwa kuzifuata nia zao wenyewe watajipatia waalimu makundi makundi, kwa kuwa wana masikio ya utafiti.” Injili 2 Timotheo 4:3

“Lakini wewe nena mafundisho yenye uzima.” Tito 2:1

Kuhusiana na ‘Mvinyo wa Babeli’, inasema: “Kwa kuwa mataifa yote wamekunywa mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake, na wafalme wa nchi wamezini naye, na wafanya biashara wa nchi wamepata mali kwa nguvu za kiburi chake.” Injili Ufunuo 18:3

Unabii wa Biblia unatuonya kwamba wakuu wa nchi watachafuliwa na huo mvinyo wa uongo uliojaa hadaa. Kwa lugha kuu ya mifano twasoma maneno haya yaliyovuviwa. Kuhusiana na siku hizi za mwisho…”wafalme wa nchi wamezini naye, nao wakaao juu ya nchi…” Ufunuo 17:2

Biblia inasema juu ya viongozi wa kitaifa wa dunia walioupokea mvinyo huo au mafundisho ya uongo ya makanisa asi yaliyoanguka, ambayo yako mengi.

Twahitaji kuyaangalia kwa makini mafundisho hayo ya Ibilisi.
Katika Injili twaonywa juu ya nyakati za hatari za siku hizi za mwisho.
“Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu; wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepusha nao.” Injili 2 Timotheo 3:1-5
Sasa tunayaanalia mafundisho machache tu kati ya hayo yapotoshayo ambayo yanaitwa ‘Mvinyo wa Babeli’.

1. Mafundisho yameenea sana yasemayo kwamba wale wanaokufa bado wanaweza kuongea na wale walio hai. Lakini Neno la Mungu latwambia kwamba mtu anapokufa anakoma kuwa hai. “Kwa sababu walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lo lote, wala hawana ijara tena; maana kumbukumbu lao limesahauliwa.”
Taurati Mhubiri 9:5 Pia Zaburi 146:4

2. Kuchanganya ibada ya sanamu katika ibada yao kwa Mungu kunakubalika kabisa. Walakini hiyo imekatazwa sana na Taurati.
“Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia. Usivisujudie wala kuvitumikia…” Kutoka 20:4-5

3. Wakristo wengi sana wanamwabudu Maryam. Walakini Neno lasema… “Usiwe na miungu mingine ila Mimi.” Taurati Kutoka 20:3

4. Mamilioni wanadai kwamba Papa wa Roma ni Badala ya au anamwakilisha Kristo. Neno lasema hivi tena, “Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu [Ruh wa Mwenyezi Mungu], ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.” Yohana 14:26

5. Makundi kwa makundi ya watu huambiwa kwamba mapokeo ya Kanisa yanaipiku Biblia. “Nao waniabudu bure, wakifundisha mafundisho yaliyo maagizo ya wanadamu.” Injili Mathayo 15:9. Masihi Isa sikuzote alilitetea Neno la Mwenyezi Mungu, yaani, Biblia, kuwa ndiyo kweli.
”Uwatakase kwa ile kweli; Neno lako ndiyo kweli.” Yohana 17:17. [Aya] hii yaihusu Taurati.

6. Makundi makubwa ya watu wanaungama dhambi zao kwa kasisi, lakini Neno litokalo kwa Mwenyezi Mungu lasema… “Nalikujulisha dhambi yangu, wala sikuuficha upotovu wangu. Nalisema, Nitayakiri maasi yangu kwa BWANA , nawe ukanisamehe upotovu wa dhambi yangu.” Zaburi 52:5

7. Vuguvugu kubwa sana la siku za mwisho litakuwa linaitukuza Jumapili kama siku takatifu ya kupumzika iliyotoka kwa Mwenyezi Mungu. Neno la Mungu lasema kwamba Sabato (Jumamosi Siku ya Saba) ndiyo siku ya kupumzika iliyowekwa na Mwenyezi Mungu mwanzoni mwa wakati na ya kwamba sheria zake takatifu ni za haki hazibadiliki.
“Ikumbuke siku ya Sabato [Jumamosi], uitakase.” Taurati Kutoka 20:8. Pia Kumbukumbu la Torati 5:15 na Nehemia 13:22 “Kuitakasa Siku ya Sabato”.

8. Makundi makubwa huambiwa kwamba wokovu waweza kupatikana kwa kutenda matendo mema au kulipa fedha. Neno litokalo kwa Mwenyezi Mungu lasema tena … “Si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyoyatenda sisi; bali kwa rehema yake, kwa kuoshwa kwa kuzaliwa mara ya pili na kufanywa upya na Roho Mtakatifu.” Injili Tito 3:5

9. Kutoa fedha ili dhambi zako zipate kusamehewa.
“Nanyi mfahamu kwamba mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo, kwa fedha au dhahabu; mpate kutoka katika mwenendo wenu usiofaa mlioupokea kwa baba zenu; bali kwa damu ya thamani, kama ya mwana-kondoo asiye na ila, asiye na waa, yaani, ya Kristo.” 1 Petro 1:18,19

10. Msamaha wa dhambi ni kupitia tu Kanisa Katoliki la Roma.
“Ambaye katika yeye [Masihi Isa] tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi.” Wakolosai 1:14

Kwa maelezo zaidi tafadhali tutembelee [tovuti}:
www.salallah.com

“Divai Safi na Takatifu”

-au-

“Mvinyo ya Babeli”

Sura 76:21 Ad-Dahr
Ufunuo 14:8

Mfululizo na..35