Kiswahili 30. Nyongeza Jesus in the Quran Kiswahili

Nyongeza 1.
Yesu katika Kurani: Orodha ya
Marejeo ya Kurani kumhusu Isa (Yesu)
Yesu/Isa ndiye “njia” (al sirat mustaqueem): 43:61.
Yesu/Isa ndiye “kweli” (al haq): 19:34.
Yesu/Isa ndiye “uzima” (Min Rouhina): 21:91, 66:12
Yesu/Isa:
Alizungumza na watu akiwa mtoto kitandani: 5:110, 19:24, 19:29-33.
Mimba yake ilikuwa kwa njia ya muujiza kupitia bikira aliyeitwa Mariamu na akawako kwa neno (fayakun): 3:47, 3:59, 19:20.

 

Mimba ilikuwa kwa uwezo wa Roho wa Mwenyezi Mungu (Rouh Al-Qudus): 21:91, 66:12.

Yeye ni Roho wa Mwenyezi Mungu (Rouh Allah): 19:17, 21:91, 66:12.
Yeye ni Roho wa/aliyetoka kwa Mwenyezi Mungu (Rouh minhu kutoka kwa Mwenyezi Mungu): 4:171.

Alitiwa nguvu/aliongozwa (ayyadhu) na Roho Mtakatifu (Rouh Qudus): 2:87, 2:253, 5:110.

Yeye na Mwenyezi Mungu wote wawili wanaitwa Bwana (rab): 9:31.
Yeye ndiye Injili au habari njema: 3:45.
Aliteremshwa (anzalata) kutoka kwa Mwenyezi Mungu: 3:53.
Aliteremshwa kutoka mbinguni (hili ni fumbo katika mapokeo ya Wasufi): 5:114-115.
Yeye ndiye Neno la Mwenyezi Mungu (kalimatu Allah): 3:39, 3:45, 4:171.
Yohana Mbatizaji anamthibitisha Yesu/Isa kuwa ndiye “Neno”: 3:39.
Mwana aliye mtakatifu, asiye na dhambi (zakiyyah): 3:46, 19:19.
Hakuwa jeuri wala mwovu: 19:32.
Hakutumia mabavu wala hakuwa mnyonge (jabbaran shakiyyan): 19:32.
Yeye ni mwenye haki (saliheen): 3:46, 6:85.
Yeye yu karibu na Mwenyezi Mungu (muqarrabeen, yaani, yuko mahali maalumu pa heshima), yeye peke yake ndiye amepewa mahali hapo katika Kurani; 3:45.

Yeye ndiye mpatanishi/mkuu/aliyetukuzwa (wajihan au wajih) sasa na hata milele. (Hii ilikuwa ni sifa ya pekee iliyotolewa tu kwa Isa na Musa, ambao kwa namna ya kuvutia sana, walikuwa ni watu wawili wanaotoa agano [ahadi]): 3:45.

Yeye ndiye mwombezi (shafa ‘a); haki ya pekee ya Mwenyezi Mungu aliyompa na kumhesabia Isa (kwa mujibu wa baadhi ya tafsiri za Wasufi): 2:255, 21:28.

Yeye ndiye njia iliyonyoka (siratun mistaqueem): 3:51, 43:61.

Amepewa siri za yale yasiyoonekana kwa macho (ghyab) (maajabu): 3:44.

Upendeleo wa Mwenyezi Mungu ulikuwa juu yake yeye: 5:110, 43:59.

Mwenyezi Mungu alimpa yeye “upendeleo” na hadhi ya nabii “zaidi ya wengine”: 2:253.

Mwenyezi Mungu alimbariki (mubarak) po pote alipokuwapo: 19:31.

Alipewa hekima na ufunuo wa Agano la Kale na Injili: 3:48, 2:36, 19:30, 43:63, 57:27.

Mwenyezi Mungu aliyadhihirisha mapenzi yake kwa Yesu/Isa: 4:163.

Mwenyezi Mungu alifanya agano [ahadi] pamoja naye: 33:7.

Yeye anafanishwa na Adamu (yeye ni Adamu wa pili): 3:59.

Aliitwa Masihi: 3:45, 4:157, 4:171, 4:172, 5:17 (mara mbili), 5:72 (mara mbili), 5:75, 9:30, 9:31.

Anakuja kuithibitisha sheria: 3:50.

Amepewa mamlaka kuhalalisha vitu vilivyoharamishwa kabla: 3:50.

Yeye ni “rehema itokayo kwa Mwenyezi Mungu” (rahmatun):19:21.

Alikuwa ishara dhahiri (be-yinat, yaani, “iliyo dhahiri na isiyo na shaka”) kwa watu (wanadamu wote): 2:87, 19:21, 21:91, 43:61.

Alionesha ishara dhahiri (be-yinat) za Mwenyezi Mungu: 2:253,3:49-50,5:114, 43:63.

Mwenyezi Mungu alimpa miujiza dhahiri: 2:253.

Alipewa uwezo wa kutia pumzi/kuumba uhai mpya kutoka katika udongo: 3:49, 5:110.

Aliwaponya vipofu na wenye ukoma: 3:49, 5:110.

Alikuwa na uwezo wa kuwafufua wafu: 3:49, 5:110.

Kwa muujiza anateremsha chakula duniani kutoka mbinguni. 5:112-118.

Watu walifanya hila (dhidi yake): 3:54.

Aliitwa “mwongo” halafu “wakamwua” (taqutulun): 2:8, 5:70.

Alikufa (mutawafeka kutokana na kitenzi cha Kiarabu tawwafa (kusababisha kifo) ambapo amutu shina lake ni mata (alikufa): 3:55, 4:159, 5:117, 19:33.

Alifufuliwa kutoka kwa wafu (yum uba’athu): 19:33, (yawezekana 6:122).

Alipaa kwenda kwa Mwenyezi Mungu mbinguni: 3:55, 4:158.

Anarudi siku ya kiama (yum al-qiyama): 3:55, 4:159, 43:61.

Yeye ni ishara ya na yeye anajua siku ya hukumu: 43:61.

Ni Mjumbe/Mtume (rasul): 4:157, 5:75.

Yeye ni Nabii (nabyyun) wa Mwenyezi Mungu: 19:30.

Yeye ni mtumishi (abd Allah) wa Mwenyezi Mungu: 4:172, 19:30, 43:59.

Yeye ni Shahidi (shahid) mwaminifu wa Mwenyezi Mungu: 4:159, 5:117.

Amani (salaam) i juu yake: 19:33.

Yeye ni kielelezo kwa wana wa Israeli: 43:59.

Aliwatia moyo wanafunzi (al-hawariyun) kuwa na imani kwa Mwenyezi Mungu: 5:111.

Wanafunzi ni wasaidizi wa Mwenyezi Mungu (ansar Allah) wanaomtangaza Yesu/Isa: 3:52, 61:l4.

Wanafunzi wake wanayo mamlaka dhidi ya adui zao: 61:14.

Wanafunzi ni mashahidi wa ukweli wa Yesu/Isa: 5:113.

Sisi tunaagizwa kumtii yeye (atee’uon): 3:50, 43:63.

Tunaagizwa kumwamini yeye (aamanou): 4:159, 5:110.

Tunaagizwa kumfuata (ettabio’un) yeye: 3:55, 43:61.

Wafuasi wake wako juu (fawqua) ya wale wasioamini: 3:55.

Wafuasi wake wanakubalika (ni waumini wa kweli) (aamanou minhum) kwa Mwenyezi Mungu: 57:27.